Sunday, August 28, 2011

BREAKING NEWS: MAFURIKO YAUA WATU ISHIRINI NCHINI NIGERIA


Hali ni tete
Magari yakiwa yamezidiwa na maji
 
 Waendesha pikipiki nao wakiokoa maisha yao



 Akina mama na watoto nao wakijaribu kuokoa maisha yao
Mvua nyingi iliyosababisha mabwawa kujaa isivyo kawaida na kusababisha baadhi ya nyumba kuzama imeua watu ishirini na kuwaacha maelfu wengine wakiwa hawana makazi huko kusini magharibi mwa Nigeria katika jiji la Ibadan, Mvua hiyo kubwa ilianza kunyesha siku ya ijumaa iliyopita.
Mafuriko hayo yayolitokana na takataka kuziba mifereji ya maji baada ya mabwawa kufurika yamesababisha kuvunjika kwa madaraja, magari kuzama na watu kutembea umbali mrefu kutoka katika maeneo yao na kwenda kutafuta hifadhi katika maeneo mengine.

No comments:

Post a Comment