Wednesday, May 30, 2012

WASHINDI WA KTMA 2012 WAAHIDI KUFANYA MAAJABU KWENYE SHOW YA DAR JUNE 2

Kiongozi wa Bendi ya African Stars(Twanga pepeta) Lwiza Mbutu akizungumza na waandishi wa habari na kuahidi kuwa watapiga show ya ajabu ambayo haijawahi kutokea
George Kavishe Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager akizungumza na wanahabari pamoja na wadau wa muziki wa kitanzania jana na kuwaalika kwenye Tamasha litaqkalofanyika katika viwanja vya Posta Sayansi jijini DSM Jumamosi hii June 2
Ikafika zamu ya Isha Mashauzi mkurya wa kwanza kuimba Taarab, nae pia ameahidi kufanya makubwa sanaaa kama kawaida yake, hivyo kama wewe ni shabiki wa Muziki wa Tanzania USIKOSEEEEEE!!!

MAMBO YA KILI TOUR MTWARA


Hapo ndo tukidondoka pande za Mtwara nikiwa na Ommy Dimpoz
Mimi, Ommy D na Dullah
Marko Killo from Eatv, Kijah na Ommy Dimpoz
Baada ya kufika nikapita Safari Radio kusalimia washikaji, hapo nikiwa na DJ Mo wa Safari Radio
Tukaenda Makonde Beach Club kwa ajili ya Interview, Roma pichani mmoja kati ya wasanii waliokamua Mtwara hapo akisubiri Interview
Team ya Eatv kabla ya kuanza Interview Makonde Beach Club kutoka kushoto ni Abdallah Ngally napenda kumuita Anko, Allan Lyimo, Olympia Fraten, Marko Killo na Happy.
Happy na Ommy Dimpoz
Nikila upepo wa Msemo Beach Hotel
Kazi ikaanza ndani ya uwanja wa Umoja kabla ya Show kuanza tukapiga Link na kuongea na baadhi ya mashabiki waliofika

Hapo ilikuwa mapema sanaaa mida ya saa saba watu walikuwa wameshaanza kuingia
After Party at New Maisha Club Mtwara
Kutoka kushoto ni Allan Lyimo alikuwa nalalamika mwenyewe eti mtwara kuna baridi ikabidi tumtafutie huo mgolole, anayefuata Kijah, Dj Mackey na Happy!! Mengi mmeyaona kwa DJ Choka na Father Kidevu Blog ila picha kamili endelea kuangalia Ting'a namba moja kwa vijana Eatv, tutakuonyesha kila kilichojiri Mtwara

Wednesday, May 23, 2012

CHARLES BABA AMSHANGAA SAJENT

Rais wa Bendi ya mashujaa musica yenye makazi yake jijini Dar es salaam, Charles Baba Kingunge (pichani juu), amefunguka kuwa namshangaa sana mzazi mwenzake Husna Idd a.k.a Sajent kwa tabia yake ya kumfuatilia na kutangaza kuwa bado ana uhusiano na mzazi mwenzake huyo wakati walishamwagana miaka miwili iliyopita. Akizungumza kupitia kipindi cha HOTMIX kinachorushwa kupitia EATV Charles alisema kuwa Sajent kwa sasa ana mpenzi wake na yeye(Charles) anaheshimu hilo lakin i anashangaa kuona mwenzake hataki kukubaliana na hilo na kumfanyia fujo kila msichana anyesikia kuwa ana uhusiano nae. Wakati huohuo Charles amekiri kumwagwa na Mlimbwende Wema Isaack Sepetu na kudai kuwa hajui sababu iliyomfanya mrembo huyo ammwage akidai kuwa labda ameona mapungufu kwake.
Husna Idd a.k.a Sajent

Friday, May 18, 2012

Tuesday, May 15, 2012

HOTMIX YA EATV PREMIER

Show mpya ya Eatv (HOTMIX) imeanza jana 14.05.2012 ikiwa na presenters wapya, kama ilivyo kawaida ya EATV yaani hawajawahi kuonekana kwenye TV yoyote hapa Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla, Show hii itakuwa inaruka kila Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia Saa 11 jioni mpaka Saa moja na itakuwa LIVEEEE
Baadhi ya wageni ambao walizindua Show yetu, (kulia ni Amani Mdimu shabiki mkubwa wa Simba SC na kushoto ni Bhoke Egina mwakilishi wa BBA Tanzania-2011)
Paul Sifael (Kushoto), Mhariri wa Ijumaa wikienda nae pia alikuwa ni mmoja kati ya wageni wetu na kushoto ni Kijah Assistant Producer wa HOTMIX
Presenters wa HOTMIX kutoka kushoto ni Fatna Ramole, Adrian Hillary na kulia ni Anna Mbajo
Baada ya show kumalizika ilikuwa ni kujifotoa tu, pichani ni Team nzima ikijifurahia baada ya kazi nzito

Sunday, May 13, 2012

HAPPY MOTHER'S DAY

(Nikiwa na jembe langu na kipenzi changu Harrison) Nakupenda na najivunia sana kuitwa mama coz kuna watu wanatamani na hawajajaaliwa, namshukuru mungu kwa kunipatia kiumbe hiki.
Nani kama mama jamani?? jibu ni hakuna... Mpende mama yako, mjali na mthamini leo wakati yupo kwa sababu siku moja hatokuwepo na utatamani awepo ili umfanyie mambo mengi sanaaa ila itakuwa Too Late... Happy Mothers day wapendwa

Friday, May 11, 2012

LUIZA MBUTU AFUNGUKA KUHUSU KUONDOKA KWA MCD

Baada ya kimya cha muda mrefu, Kiongozi wa Bendi ya African Stars (Twanga pepeta) Luiza Mbutu (Pichani juu) amefunguka kuhusu kuondoka kwa aliyekuwa mpiga tumba wa muda mrefu katika bendi hiyo (MCD) na kujiunga na Bendi ya Mashujaa Musica. Akizungumza na blog hii Luiza amesema kuwa kwa upande wake yeye kama kiongozi wa Bendi na mtu aliyefanya nae kazi kwa muda mrefu amesikitishwa sana na hapendi kuona mtu akiondoka kwenye bendi hiyo lakini hawezi kumzuia mtu kufanya kile anachofikiria ikiwa ni pamoja na kuhama bendi na kuongeza kuwa wakati wowote yeye(MCD) na wanamuziki wengine walioihama Bendi hiyo wakijisikia kurudi wanakaribishwa kama walivyomkaribisha Muumini Mwinjuma, Badi Bakule na wengineo ambao waliondoka na kurudi.



Naye aliyekuwa mwanamuziki wa zamani wa Bendi ya African Revolution(Tamtam) iliyokuwa ndugu na African Stars ambaye sasa amejiunga na Bendi hiyo ya African Stars Badi Bakule(Pichani juu) amesema ameamua kujiunga na Bendi hiyo kwa kuwa anachukulia kama nyumbani kwa kuwa kampuni ya Asset inayomiliki Bendi hiyo ndiyo iliyomtoa na kumpa umaarufu mkubwa kipindi cha nyuma hivyo ameamua kurudi nyumbani baada ya kugundua kuwa kipaji chake kinapotea kwa kuwa Bendi za T.O.T na Laventure Musica alizokuwa akifanya nazo kazi kabla ya kuamua kujiunga na Twanga zilikuwa hazifanyi maonyesho na kufanya mashabiki wake wasimsikie tena..Hata hivyo mahojiano haya utayaona Liiiveee kupitia Kipindi cha Afrobeat, kaa tayari.


AFROBEAT KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAMA DUNIANI-MAY 13

Hapo nikiwa on Set kwa ajili ya maandalizi ya Show yangu ya Afrobeat Jumamosi hii
Swagga zikiendelea, nikijiweka Fit kabla ya kuanza Show.. Dressed by Kim Ladies Wear Boutique Kinondoni kona ya kuelekea mwananyamala, mnakaribishwaaaa.
Kuelekea maadhimisho ya Siku ya mama duniani, kwa kutambua kuwa kuna wamama wengi Afrika ambao wamepata mafanikio na heshima kubwa sana katika jamii yao na Dunia kwa ujumla, ndani ya Afrobeat wiki hii tunazungumzia Historia ya mwanamama Yvonne machaka a.k.a Chakachaka kwa ufupi tu lakini pia tutaangalia yale machache ambayo ameyafanya kwa waafrika wenzake  hasa akina mama na watoto katika suala zima la afya kwa kutumia nguvu aliyonayo kama mwanamuziki pia kama Balozi wa Umoja wa mataifa katika kupambana na malaria.
Ni jumamosi hii saa moja jioni... USIKOSEEE!!!

KUELEKEA SIKU YA MAMA DUNIANI MAY 13, TUPAMBANE NA UNYANYASAJI WA WANAWAKE

Mapenzi haya ni ya kizamani jamani, mwanamke hapigwi kwa ngumi hupigwa kwa maneno matamu yenye upendo na wengine husema mwanamke hupigwa kwa kitenge cha Wax
Huyu kamwagiwa maji ya moto na mume wake eti kisa kamnyima unyumba, sasa baada ya kummwagia maji na kumjeruhi kiasi hiki ndo alipewa huo unyumba? Jamani wanaume kama mkeo/mpenzi wako hajisikii kufanya tendo hilo na unaona huna jinsi umezidiwa basi mpe maneno matamu mkeo/mpenzio ya kumshawishi na kumlainisha ili akuelewe siyo kumfanyia matendo ya kinyama namna hii.. Huu ni unyanyasaji, wanawake kwa pamoja tushirikiane kuutokomeza unyanyasaji wa namna hii.
Hivi baada ya kitendo kama hiki unawezaje hata kunuangalia usoni tena mkeo? Tujitahidi kuzuia hasira zetu na kama amekushinda basi muachane kwa usalama na siyo kutiana vilema visivyo na sababu..... Picha: kwa hisani ya

MCHEZAJI WA ZAMANI WA MAN U QUINTON FORTUNE ATEMBELEA EATV & RADIO

Mchezaji wa zamani wa Manchester United Quinton Fortune akizungumza na waandishi wa habari wa Eatv na EARadio alipotembelea katika Studio hizo jana
Quinton (kulia) na Kijah
Quinton akiwa na mtangazaji wa Kipindi cha michezo cha Capital Radio, Master Tindwa

Thursday, May 3, 2012

BIG BROTHER AFRICA MWAKA HUU KUANZA MAY 6

Hii ni moja kati ya sehemu za Jumba la Big Brother mwaka huu ambayo itafahamika kama Big Brother Star game, inayotarajiwa kuanza May 6 mwaka huu huko Afrika kusini ambapo mwanamuziki J. Cole ataperform Live.
Show hiyo itakuwa ikionyeshwa masaa 24 kuanzia May 6 saa 3 usiku kwa muda wa siku 91 kupitia Channel 198 za DSTV.

MFAHAMU TANZANIA ONE(MSICHANA ALIYEONGOZA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2012

Anaitwa Faith Asenga(Ndiye msichana aliyeongoza katika matokeo ya kidato cha sita mwaka huu)
Leo alikuja katika ofisi za Eatv kwa ajili ya mahojiano na kipindi cha  Breakfast cha East Africa Radio, nasi wengine pia tulipata nafasi ya kuzungumza nae, kikubwa zaidi amesema kuwa mpaka hapo alipofika ni jitihada zake mwenyewe ndizo ambazo zimezaa matunda hayo kwa kuwa alikuwa anajua umuhimu wa Elimu hivyo kwa kutambua hilo ilimbidi ajitume sana na kuweka nia ya kufanya vizuri katika masomo yake ili aweze kutimiza ndoto zake za kuwa Civil Engineer kama mungu akimjaalia maana hilo ndilo lengo lake kubwa sana na ndilo lililomsukuma yeye kuchukua mchepuo wa Sayansi, pamoja na mengi aliyozungumza pia amewataka wanafunzi wenzake kuwa na ushirikiano, waheshimu kila mtu wao kwa wao, wazazi wao na waalimu pia maana heshima ndiyo msingi wa kila kitu na mwisho amewataka wajitume na wawe na ndoto za kuwa watu fulani(Pichani juu akizungumza na Allan Lucky wa Skonga)
Faith hakuja peke yake(Pichani juu ni yeye "Faith" na wazazi wake) pia na wao walizungumza ya kwao ambapo wamewataka wazazi wenzao waige mfano wao kwa kuwa karibu na mtoto wao, wawape ushirikiano wa kutosha na kufuatilia maendeleo yao shuleni.Aidha wameongeza kuwa wamepata faraja kubwa kwa matokeo ya mtoto wao kwani wanaamini yeye kama msichana amepitia changamoto nyingi sana lakini ameweza kuzivuka hivyo wasichana wengine waige mfano wake.

SHINDANO LA MISS TABATA KUFANYIKA JUNI 1-DAR WEST PARK TABATA

  Warembo wanaowania Taji la Miss Tabata katika picha ya pamoja 
Shindano la kumsaka mrembo wa Tabata, Miss Tabata 2012, litafanyika Juni 1 mwaka huu katika ukumbi wa Da West Park, Tabata.
Mratibu wa shindano hilo Joseph Kapinga amesema kuwa katika onyesho hilo pia kutakuwa na sherehe kabambe ya kusherehekea miaka 10 ya Miss Tabata.

“Shindano la mwaka huu litakuwa ni la aina yake kwa sasabu hii itakuwa ni mwaka wetu wa 10 kuandaa shindano hili la Miss Tabata hivyo tutakuwa na burudani nyingi kutoka nje na ndani ya nchi. Pia tutahakikisha tunashirikisha warembo bomba wenye hadhi ya kushinda taji la Miss World,” Alisema Kapinga mratibu wa Bob Entertainment na Keen Arts.
Aidha Kapinga alisema kuwa warembo waliowahi kushinda mataji tofauti tofauti ya shindano hilo pia watakuwepo kusherekea miaka 10 ya Miss Tabata.
Warembo watakaoshiriki kwenye shindano wanaendelea na mazoezi kila siku katika ukumbi wa Dar West Park.

Wednesday, May 2, 2012

TOK-ELEZEIYER INTER-SCHOOL CONCERT @KENTON HIGH SCHOOL

12th May, 2012 (10am - 6pm)

Brought To You By:
Friends 4 Friends Group

In Collaboration With:
Waka Waka Na Coca-Cola
New Timbaland Collections
Kali Elegance


Hosted By:
Allan Lucky (Students' President, The Luckiest Dude Alive);
DJ AD (Mafuvu);
Tonny (TBway360) & Faiza (Baby Drama)

Entrance:
7,000/= Prior; 10,000/= @The Gate

Special Appearances:
Dully Sykes, Cyril Kamikaze, Mtu Che (YoungDSM, Stamina, CountryBoy)

Activities:
Hip-Hop Battles, Dancing & Singing Competitions, Q & A, Dogue Competition, Fashion Show & So Much More!

Contacts:
+255717516171 (Agape Daniel Ex-Tusiime);
+255715765396 (Deo Komba Ex-Tusiime);
+255712056765 (Victor Baraka Ngowi Ex-St Anthony's)

DK. MAHANGA AIBUKA KIDEDE KATIKA KESI YA KUPINGA USHINDI WAKE KATIKA UCHAGUZI MKUU MWAKA 2010

Habari kutoka Mahakama kuu jijini Dar es salaam zinasema kuwa Mbunge wa Jimbo la Segerea kwa tiketi ya CCM, Dk. Milton Makongoro Mahanga(Pichani juu) ameshinda kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea mwenzake kupitia tiketi ya Chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA) Bw. Fred Mpendazoe, kupinga ushindi wake katika Jimbo hilo la Segerea wakati wa uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Dk. Makongoro akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hukumu kutolewa
Wafuasi wa Dk. Mahanga wakimpongeza kwa ushindi
Wafuasi wa Chadema pia walikuwepo mahakamani hapo
Dk. Mahanga akiwapungia wafuasi wa CCM


Picha kwa Hisani ya Michuzi blog

WAVULANA WAPASUA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA

                                                           Dk. Joyce Ndalichako
 
BARAZA la Mtihani la Tanzania (Necta), limetangaza matokeo ya mitihani ya kidato cha sita iliyofanyika Februari mwaka huu yakionyesha kuongezeka kidogo kwa kiwango cha ufaulu kwa ujumla huku wavulana waliofaulu wakiwaacha mbali wasichana.

Katika matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Joyce Ndalichako (pichani), kati ya watahiniwa 46,499 waliofanya mtihani huo, wavulana waliofaulu ni 30,466 wakati wasichana ni 16,033. Hata hivyo, kumekuwa na mchuano mkali katika ufaulu kwa asilimia ambao wasichana walipata 87.37 na wavulana 87.69.

Sekondari ya Wasichana ya Marian, Bagamoyo ndiyo iliyoongoza kitaifa na mwanafunzi wake, Faith Assenga ndiye aliyeshika namba moja katika masomo ya Sayansi.

“Katika masomo ya Biashara, aliyeshika nafasi ya kwanza ni Alex Isdor wa Sekondari ya Kibaha na Lugha ni Faridi Abdallah wa Sekondari ya Mpwapwa,” alisema Dk Ndalichako.

Dk Ndalichako alisema kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa 46,499; wakiwemo wale wa kujitegemea, kimeongezeka kutoka asilimia 87.24 mwaka jana hadi 87.58 mwaka huu.
 
                                                      Zaidi bofya hapa

Tuesday, May 1, 2012

MAANDALIZI KABLA YA SHOOTING


Makeup inahusika zaidi kwenye screen, hapo makeup Artist wangu Irene Moshi akihakikisha natokelezea poa Runingani
Baada ya Makeup sound man Timothy Chelula (TC) nae akiplay party yake hapo akinifunga Mic ili mambo yaanze
Hapo mwenyewe nikajua niko sawa tayari kwa kuanza show, sasa subiri uone kilichotokea picha ya chini
Irene mwenyewe akasema hapana bado kuna kitu hakijakaa sawa ikabidi arudi kurekebisha... Nimejaribu kukuwekea hii ili uone tu mambo yanavyokuwa hadi kipindi kikamilike, siku nyingine nitakuwekea Production Team nzima leo nimekuonjesha tu