Friday, October 19, 2012

Wolper aathiriwa na Uchumba

    
                               
                               Jacqueline Wolper katika moja ya pozi zake


Ni yule Msanii  kutoka kiwanda cha filamu Bongo,  Jacqueline Wolper  amesema kutokana na tabia aliyoonesha aliyekuwa mchumba wake, Abdallah Mtoro ‘Dallas’ amekoma na hatorudia kumtangaza mchumba hadharani.

Akizungumza na kituo kimoja maarufu cha runinga jijini Dar juzikati, Wolper alisema amejifunza mengi kutokana na tabia aliyoionesha Dallas baada ya kumtangaza kuwa ni mchumba wake.

“Dallas alipokuwa mbali alionesha mapenzi ya dhati ndiyo maana nikampenda na nikamtangaza hadharani lakini alipokuja karibu tabia zake hazikunifurahisha ndiyo maana nikamuacha,” alisema Jacgueline.

No comments:

Post a Comment