Friday, October 26, 2012

TINO ATANGAZA KUACHANA NA FILAMU ZA MAPENZI

Msanii nguli wa filamu nchini Hisani Muya maarufu kama Tino anatarajia kuzindua Movie yake mpya aliyoipa jina la CID ambayo imefanywa kwa style ya "Action" zaidi.
Uzinduzi huo unaotarajiwa kufanyika leo katika ukumbi wa Business Park uliopo Victoria utafuatiwa na Uzinduzi wa Project yake mpya ya kusaka vipaji vya waigizaji wachanga yaani Movie Star Search.
Akizungumza na Blog hii Tino amesema ameamua kuanzisha Project hiyo baada ya kugundua kuwa kuna vipaji vingi sana mtaani lakini vinashindwa kuibuliwa kutokana na vijana hao kukosa nafasi ya kuonyesha vipaji vyao hivyo.
Pamoja na uzinduzi wa Filamu na Project yake hiyo pia Tino atatangazwa rasmi kuwa Balozi wa kituo kimoja cha watoto Yatima kilichopo wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.
Aidha Tino amefunguka kuwa kuanzia sasa ameachana Rasmi na Filamu za mapenzi na kujikita zaidi kwenye filamu za Action.

No comments:

Post a Comment