Monday, October 22, 2012

DAR LIVE YACHANUA NA MSAKO WA THE MIC KING, TMK WANAUME NA EXTRA BONGO

Si lingine bali ni lile shindano la kumsaka Mfalme wa Mic (The Mic King), AfroKija bila kuchelewa ilikuwa ndani ya tukio lililowika ndani ya Ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem na kuwapa wawakilishi wapatao 12 wa Wilaya ya Ilala, huku burudani ya kufa mtu ikishushwa na Kundi zima la Wanaume TMK ikiwemo na Bendi ya Exrta Bongo.

                      

Kundi zima la TMK Wanaume likionyesha staili yao ya Mapanga Shaaa jukwaani.


 
Washiriki 12 waliopenya katika shindano hilo wakiwakilisha wilaya ya Ilala.

Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo, Ali Choki (kulia) akiwa na wanenguaji wake jukwaani.

 
Memba mzee wa kundi hilo, Bibi Cheka (kushoto) akimwaga mistari jukwaani. Kulia ni Temb


Mmoja wa washiriki wa The Mic King akionyesha uwezo wake jukwaani.

...The Mic King akiendelea kusakwa.

Majaji wa The Mic King, Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’ (kushoto), John Dilinga ‘DJ JD’, na Sister P wakifuatilia shindano hilo.

 Mmoja wa washiriki akionyesha ufundi wa kurap.


Wanenguaji wa Extra Bongo wakionesha mambo jukwaani kuinogesha Dar Live.

Msanii anayesumbua na songi la Mwanayumba ndani ya gemu la Bongo Fleva, Chegge Chigunda, akimsaka ‘Mwanayumba wake’ jukwaani.

 Mkali wa kundi wa TMK Wanaume, Amani Temba, akiwaimbisha mashabiki wake kwa kutumia kipaza sauti.

                                       
          Zao jipya la Kundi la TMK Wanaume, mwanamuziki    
                     Getruda, akionyesha  uwezo wake jukwaani.

No comments:

Post a Comment