Wednesday, October 17, 2012

WAFUASI WA KUNDI LA UAMSHO WAFANYA VURUGU ZANZIBAR NA WENGINE WAANDAMANA KITUO CHA POLISI KATI DSM



Pichani juu baadhi ya matukio yaliyotokea zanzibar mchana wa leo
Siku chache baada ya watu wanaosadikiwa kuwa ni Waumini wa dini ya kiislamu kufanya vurugu kufuatia mtoto mmoja kukojolea kitabu cha Qur'an na kusababisha jeshi la polisi kuwakamata watuhumiwa zaidi ya 37 na kuwafikisha mahakamani, leo limeibuka jipya baada ya watu wengine wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa Sheikh Issa Ponda kuandamana kuelekea katika kituo cha Polisi kati jijini Dar Es Salaam.
Watu hao wameandamana kupinga kukamatwa kwa katibu wa Jumuiya na Taasisi ya kiislam Sheikh Issa Ponda ambaye alikamatwa jana usiku na kushinikiza aachiwe huru, wamesababisha askari Polisi kutanda katika eneo hilo na kulazimika kutumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu hao ambao hata hivyo walionekana kukataa kuondoka katika eneo hilo mpaka Katibu wao huyo aachiwe huru.
Sheikh Ponda amekamatwa kufuatia tuhuma mbalimbali zikiwemo za kuhusika na uchochezi kwa serikali iliyopo madarakani na kuchochea vurugu za udini baina ya waislam na wakristo likiwemo tukio lile la Mbagala lililotoke hivi karibuni Mbagala jijini DSM.
Wakati huo huo wafuasi wa kundi la uamsho wamefanya vurugu kufuatia kile kilichodaiwa kuwa ni kutekwa kwa kiongozi wao wa kundi la uamsho, jambo lililowalazimu Polisi kutumia mambomu ya machozi kuwasambaratisha wafuasi hao.

No comments:

Post a Comment