Monday, April 23, 2012

MASHUJAA MUSICA YAZIDI KUIBOMOA TWANGA, WALETA MZIGO MPYA KUTOKA EXTRA BONGO

Bendi ya muziki wa dansi nchini, Mashujaa musica iliyokuja na style ya kukomba wanamuziki kutoka katika Bendi mbalimbali nchini, baada ya kuivuruga Bendi kongwe ya Twanga Pepeta  na kuchukua wanamuziki wake tegemezi kama Charles Baba na Lilyan Internet imeendeleza vurugu zake kwa Bendi hiyo ambapo sasa imetangaza kumnyakua Mpiga Drums tegemezi wa Bendi hiyo maarufu kama MCD (pichani juu)
Akizungumza na Blog hii mkurugenzi wa bendi hiyo Max Luhanga akiwa njiani kuelekea Morogoro kwa shughuli za kikazi amesema, bado wanaendelea na mchakato wa kuimarisha bendi yao ambapo pia wamemchukua Rapa maarufu wa Bendi ya Extra Bongo anayefahamika kwa jina maarufu la Ferguson (pichani), na kuongeza kuwa kila kitu kimeshakamilika kilichobaki ni kusubiri utambulisho rasmi ambao utafanyika Ijumaa ya April 27 katika ukumbi wa Business park uliopo Victoria jijini Dar es salaam.. Kaa kushuhudia uzinduzi huo kupitia Afrobeat ya Eatv, Stay tuned.



No comments:

Post a Comment