Wednesday, April 11, 2012

VICENT KIGOSI (RAY) ALIA NA WANAOMSEMA VIBAYA KUHUSU UHUSIANO WAKE NA MAREHEMU STEVEN KANUMBA

Mmoja kati ya wacheza filamu wakubwa nchini, Vicent Kigosi(Ray) ameezungumzia namna anavyoguswa na kuumizwa na maneno yanayosemwa na watu kuhusiana na tofauti zilizokuwepo baina yake na marehemu Steven Kanumba ambao kabla ya tofauti hizo walikuwa ni marafiki wakubwa na kufikia hatua ya kuitana "Swaiba" na pia majina ya The Great bna The Greatest" yalitokana na uswaiba huo waliokuwa nao.

Akielezea kwa uchungu namna alivyoguswa na kifo cha Swaiba wake huyo na tofauti ya yale watu wanayoyazungumza kupitia Blog yake, Ray amesema "mengi yanazungumzwa juu yangu ila kila kitu mimi namuachia Mungu mimi ni mnyonge siwezi kupambana nanyi mnaoniongelea vibaya maumivu nayoyapata juu yenu Mungu hatowaacha siwezi kuzizuia hisia zenu kuzungumza yale mnayojisikia."

Aidha Ray ameonyesha kutubu kwa yale yote yaliyotokea kati yake na Kanumba na kusema" yote yaliyotokea ni kawaida ya binadamu kutoelewana, kama Baba na Mama wanafunga ndoa kanisani na wanakula viapo vya utii mbele za Mungu lakini wanagombana na kufikia hatua ya kuachana kwanini ishindikane kwetu ni hali ya kawaida katika maisha binadamu kutofautiana.

1 comment:

  1. Siku zote sio binadamu wote watakaokusema kwa mazuri kaka kaza moyo mwombe mungu akusaidie kusonga mbele kaka

    ReplyDelete