Thursday, April 19, 2012

TWANGA PEPETA YAMNYAKUA BADI BAKULE


Muda mfupi baada ya Bendi ya Levent Musica iliyokuwa na makazi yake mjinimorogoro kusambaratika, Mmoja kati ya waimbaji wake Badi Bakule (pichani) amerejea jijini Dar es Salaam na kujiunga na Bendi ya African Stars (Twanga pepeta).

Meneja wa Bendi hiyo Hassan Rehani amesema mwimbaji huyo amejiunga na Bendi hiyo mwanzoni mwa wiki hii na wanatarajia kuanza kumtambulisha Rasmi Kesho Ijumaa katika ukumbi wa Africenter-Ilala na baadae watafanya utambulisho mwingine siku ya Jumamosi katika ukumbi wa Mango garden Kinondoni.

Rehan ameongeza kuwa wamemchukua Badi Bakule kutokana na uwezo wake katikautungaji na uimbaji ambapo ameziba pengo la muimbaji wa sauti ya tatu ambayo haina mwimbaji wa kutegemewa.

Mengi zaidi kuhusiana na Badi Bakule kuhamia Twanga pepeta utayapata kupitia Afrobeat wiki ijayo.... Usikoseeeeeeeee!!!!

No comments:

Post a Comment