Thursday, April 12, 2012

BAADA YA MAMA LULU SASA NI BABA LULU

Baba mzazi wa Elizabeth Michael "Lulu"
Baba mzazi wa muigizaji wa kike wa fialamu nchini maarufu kama Lulu, ambae anahusishwa na kifo cha marehemu Steven Charles Kanumba ameibuka na kueleza kushtushwa sana na taarifa za kifo hicho pamoja na habari kuwa bintiye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na muigizaji huyo nguli na kuhusishwa na kifo chake.

Baba Lulu ambaye alijitambulisha kwa jina la Michael Edward Kimetameta(49) mzaliwa wa wilaya ya Rombo, mkoani kilimanjaro amesema kuwa alimtambua Steven Kanumba kama mwalimu wa mwanae lakini hakuamini masikio yake pale alipopata taarifa za kifo hicho huku bintiye anayedaiwa kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na marehemu, anahusika.

Zaidi ingia hapa

No comments:

Post a Comment