Tuesday, April 10, 2012

MAELFU YAFURIKA KUUAGA MWILI WA MAREHEMU STEVEN KANUMBA

Maelfu ya watu waliohudhuria katika shughuli ya kuaga mwili wa Steven Kanumba(Hapo ni wakati mwili wa mwrehemu ukiondoka Leaders na kuelekea makaburi ya kinondoni alipozikwa)

Makamu wa Rais Dk Bilal akiongoza maelfu waliojitokeza kuuaga mwili wa Steven kanumba

Mke wa Rais mama Salma Kikwete akiuaga mwili wa marehemu

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa Mh. Benard Membe nae akiuaga mwili wa marehemu

Mbunge wa Mbeya mjini Mh. Joseph Mbilinyi(Sugu) naye akitoa heshima zake za mwisho kwa marehemu Steven Kanumba

Mmoja kati ya waigizaji wa siku nyingi na mtu wa karibu wa kanumba Dino, akielezea machache kuhusu mazishi ya kanumba na kwa upande wake ameelezea kama ni tukio la kihistoria, wakati akifanya mahojiano na EATV.
Askari wa jeshi la Polisi wakihakikisha hali inakuwa salama
                                                
Watu walithubutu kupanda juu ya mti ili mradi waushuhudie mwili wa marehemu kanumba kwa mara ya mwisho






Nilikuwepo pia kwa ajili ya kuripoti yaliyokuwa yakiendelea kwenye mazishi hayo.

Ndugu zetu wa chama cha msalaba mwekundu(Red Cross) walifanya kazi kubwa sana, maana watu wengi sana walikuwa wakidondoka.. Kwa kweli watu wengi sana alijitokeza kumuaga na kumzika marehemu Steven Kanumba na kila mmoja alionyesha kuguswa kwake kwa msiba huu ila mwisho wa siku tunaamini kuwa mipango ya mungu haina makosa kilichobaki tumuombee tu alale mahali pema peponi.. Amina.

No comments:

Post a Comment