Wednesday, April 4, 2012

HUKU IKISHANGILIA USHINDI DHIDI YA BLACKBURN ROVERS MAN U YAPATA PIGO


Pamoja na kuendelea kubaki kileleni mwa ligi kuu ya England baada ya kuibamiza Blackburn Rovers bao 2-0 juzi, Klabu ya Mashetani wekundu Manchester United imejikuta ikipatwa na majonzi kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi wa zamani wa Klabu hiyo Amer Midani.
 
Midani ambae ni mzaliwa wa Beirrut alijiunga na Klabu hiyo mwaka 1987 wakati Klabu hiyo ya Old Trafford ilipoinunua klabu ya mpira wa kikapu ya Manchester Giants ambayo Miadi alikuwa mwenyekiti wake.
 
Hapo awali Midani alikuwa raia wa Lebanon na bingwa wa michuano ya watoto ya table tennis akiwa na umri wa miaka 15 na ambapo baadae alihamia England akiwa ana umri wa miaka 18.

No comments:

Post a Comment