Wednesday, April 11, 2012

TAARIFA YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA KWA WATANZANIA KUHUSU TSUNAMI

Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania imetoa tahadhari kuwa kutakuwa na tetemeko la ardhi(Tsunami) ambayo yanahofiwa kufika kwenye pwani ya Tanzania hasa katika maeneo ya Mkoa wa Mtwara kuanzia saa 11 jioni ya leo.

Tetemeko hilo lililotokea chini ya Bahari na kutarajiwa kutengeneza mawimbi ya Tsunami limeanzia huko Sumatra nchini Indonesia.

Aidha katika taarifa hiyo Mamlaka imewaomba wananchi kuchukua tahadhari na kufuatilia taarifa katika vyombo vya habari ili kufahamu hali inaendeleaje kwa kuwa watakuwa wanatoa taarifa mara kwa mara pia wamewataka wananchi wanaoishi sehemu tambarare mawimbi yanaweza kuingia ndani ila sehemu za miinuko wanaweza wasipate athari.

No comments:

Post a Comment