Sunday, April 15, 2012

KILIMANJARO MUSIC AWARDS 2012 DIAMOND ARUDI KILELENI ANYAKUA TUZO TATU

Umati wa watu waliojitokeza kushuhudia nani ataondoka na nini

Washereheshaji wa usiku huo walikuwa ni Millard Ayo( kushoto) na Vanessa Mdee


Bi Shakila, Patricia Hllary kutoka Bendi ya JKT pia walikuwepo kutoa burudani usiku huo

Mpoki alituvunja mbavu zetu na kutuongezea siku za kuishi, yaani ilikuwa burudani ya kutosha sana

Queen Darleen (katikati) alijinyakulia Tuzo ya wimbo bora wa Dancehall kushoto kwake ni Taji Liundi na Kulia ni Abby waliomkabidhi Tuzo hiyo

Kushoto ni Mtangazaji mkongwe na kipenzi cha watu wengi sana Reinfred Masako kutoka ITV/Radio One na Dina Marios wa Clouds Fm wakimkabidhi Tuzo ya wimbo bora wa zouk/Rhumba mwanamuziki Ally Kiba, anayeshuhudia mwenye gauni nyeusi ni mdogo wake Ally Kiba.

Mwanamuziki AT akichukua Tuzo yake ya wimbo bora wenye vionjo vya asili aliyemsindikiza ni Mwanne aliyeshirikiana nae kwenye wimbo huo na mwenye suti ni Shelukindo na Angela Damas waliomkabidhi Tuzo hiyo

Mwanamuziki anayekuja juu kwenye muziki wa Taarab Isha Ramadhan(Mashauzi) akipokea Tuzo yake ya wimbo bora wa Taarab

Mzee Kalala kama haamini anachokisoma vileee, yuko na Shamim wa 8020 Fashions blog, wao walitoa Tuzo ya wimbo bora wa kiswahili(Bendi) Tuzo iliyoenda kwa Twanga pepeta kupitia wimbo dunia daraja utunzi wa Charles baba ambaye sasa hivi yuko Mashujaa

Malkia wa mipasho Afrika mashariki Khadija Omary Kopa, aliyenyakua Tuzo ya mtumbuizaji bora wa kike akiwa pamoja na binti zake na mume wake ambao walikuja kumpa Support usiku huo
Kiongozi wa bendi ya Twanga pepeta Luiza Mbutu akiwashukuru mashabiki kwa niaba ya Bendi
Diamond ambae amerudisha heshima yake kwa kuchukua Tuzo 3 katika Tuzo za mwaka huu baada ya mwaka jana kuambulia patupu akiwa na wapambe wake baada ya kuchukua Tuzo ya pili, mwenye gauni ya purple ni mama yake mzazi.

No comments:

Post a Comment