Monday, November 26, 2012

TAARIFA YA KIFO CHA MSANII SHARO MILIONEA KUTOKA KWA KAMANDA WA POLISI MKOA WA TANGA

Sharo Milionea enzi za uhai wake
Namkariri Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Constantine Massawe akizungumza na East Africa Radio jana usiku akisema, “leo majira ya saa mbili usiku kwenye barabara ya Segera Muheza mtu mmoja alietambulika kwa jina la Hussein Ramadhani au Sharo Milionea akiwa anaendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es salaam kwenda Muheza alipofika eneo la Maguzonizonga wilayani Muheza hilo gari lake liliacha njia na kupinduka mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”

Kamanda amesema hakuna kona kali sana wala ubovu wa barabara kwenye sehemu aliyopata ajali Sharo Milionea, katikati ya Segera na Muheza ambapo gari imehifadhiwa mahali salama kwa sababu haitembei.
Kwenye gari alikuwa mwenyewe hivyo hakuna taarifa kamili ya nini kilichotokea maana inaweza kuwa alisinzia.

R.I.P Sharo tulikupenda lakini mungu kakupenda zaidi, kazi zako tulizipenda na tutakukumbuka kwa mengi.

No comments:

Post a Comment