Wednesday, November 7, 2012

MAMA MZAZI WA RAY C AFUNGUKA KUHUSU MWANAE, AOMBA MSAADA KWA WATANZANIA NA MASHABIKI WA RAY C

Siku chache baada ya vyombo vya habari kuripoti kuwa mwanamuziki Ray C (kiuno bila mfupa, pichani chini) ameathirika kwa kutumia madawa ya kulevya, mama mzazi wa msanii huyo (pichani juu)  amejitokeza na kuomba msaada kwa ajili ya matatizo ya mtoto wake.
Akizungumza na kipindi cha Hotmix kinachoruka kupitia Eatv mama huyo amefunguka kuwa ni kweli kuwa mtoto wake huyo ameathirika kutokana na matumizi ya dawa za kulevya na kuwataka waandishi wa habari kutoandika habari zitakazomkatisha tamaa msanii huyo, watu waliojitolea kumsaidia na familia yake kwa ujumla.
Aidha mama huyo ameongeza kuwa tatizo lililompata Ray C linaweza kumpata mtu yeyote hivyo amewaomba mashabiki wake kuelewa tatizo hilo na waendelee kumuombea na kumsaidia ili aweze kupona na kuondokana na matumizi ya dawa hizo kabisa.
Mama huyo amewaomba wasamaria wema na mashabiki wa msanii huyo wenye uwezo kujitokeza na kumsaidia mama huyo pesa kwa ajili ya kumuuguza mwanae kwa kuwa dawa anazotumia ni za gharama kubwa hivyo yeye peke yake hawezi kumudu kuzinunua.

Kwa mawasiliano zaidi na mchango waweza wasiliana na mama huyo kwa simu namba 0655 666700

No comments:

Post a Comment