Wednesday, November 14, 2012

PUMZIKA KWA AMANI LULU WETU

Pichani juu na chini ni marehemu Lulu Oscar wakati wa uhai wake
Aliyekuwa mwandishi wa habari na mtangazaji wa kituo cha SIBUKA TV, aliekuwa akitangaza kipindi cha Pepeta afrika, Lulu Oscar (pichani)amefariki dunia jana nyumbani kwao Mbezi Kwa Yusufu.

Akizungumz na blog hii, mdogo wa marehemu, Ritha Oscar alisema kuwa Lulu alipatwa na mauti hayo majira ya usiku ambapo alizidiwa ghafla kufuatia kulalamikia kifua kumbana.

Siku chache zilizopita alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya Masister ya Luguluni Mbezi, zaidi ya mara tatu, baadae aliruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kuendelea vizuri lakini juzi usiku alilalamikia kifua kikimbana tulimuhangaikia mpaka hatua ya mwisho lakini ikashindikana na alipoteza maisha” alisema Ritha huku akilia.

Aidha, alisema kuwa, ndugu baada ya kukutana wamekubaliana kuuzika mwili wa marehemu siku ya Alhamisi(kesho) katika Makaburi ya Kinondoni na msafara utaanzia nyumbani Mbezi kwa Yusufu na kuelekea Makaburini.

Katika historia yake, Lulu alihitimu elimu yake ya msingi mwaka 1996 katika shule ya Upanga pia ana elimu ya uandishi wa habari aliyoipata chuo cha uandishi wa habari na utangazaji (Royal College of Tanzania) aliyohitimu mwaka 2009 ambapo mwaka 2003,  alihitimu kozi ya elimu ya juu katiika Taasisi ya uandishi wa habari na mawasiliano Institute of journalisim and mass communication DSM.

Nimesikitishwa sana na kifo cha Lulu kwani pamoja na kwamba nilisoma nae lakini tulikuwa tukiwasiliana mara kwa mara kwa kuwa tulikuwa tukifanya vipindi vinavyofanana na mara nyingi alikuwa akinipigia na kuniomba namba za wasanii mbalimbali wa muziki wa dansi, na mara ya mwisho tuliwasiliana wiki mbili zilizopita akiniomba namba ya mwanamuziki na Rais wa mashujaa musica Charles Baba.


Tulikupenda sana Lulu lakini mungu amekupenda zaidi, Pumzika kwa amani ndugu yangu, rafiki yangu  mbele wewe nyuma sisi.

Mwenyezimungu aiweke roho yako mahali pema peponi.. Amina.

No comments:

Post a Comment