Thursday, November 22, 2012

KIJANA HUYU ANAHITAJI MSAADA WAKO


Kijana Swakimu Elius mwenye umri wa miaka 14 mkazi wa Mtwara anahitaji msaada wako wa hali na mali kutokana na maradhi ya uvimbe usoni yanayomkabili.
 
Akizungumza kwa shida katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikolazwa kijana huyo, Swakimu amesema
 
“Ugonjwa huu ambao sijui chanzo chake umekuwa ukinitesa sana na kunifanya nishindwe kuendelea na masomo katika Sekondari ya Libobe, Mtwara.

“Uvimbe unaonitesa ulianza kama kipele lakini kadiri siku zilivyokuwa zikisonga mbele uliongezeka ndipo nilikwenda Hospitali ya Mkoa wa Mtwara ambapo walinitibu kisha waliniambia nije hapa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

“Kinachonihuzunisha sina msaada wowote kwani ndugu yangu aliyenipokea hana uwezo na ninatakiwa kutoa gharama za matibabu shilingi 90,000 na damu,” alisema mtoto huyo.

“Nawaomba Watanzania wanisaidie kiasi hicho cha fedha na damu ili nifanyiwe upasuaji ambao nimeelezwa na madaktari kwamba utaisha na kuwa na afya njema,” alieleza Swakimu kwa uchungu.

Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi wa Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili, Mary Ochieng aliomba kijana huyo asaidiwe kwa kuwa hana ndugu wa kumsaidia.

Yeyote atakayeguswa na maradhi ya kijana huyu aende wodi namba 23 Sewa Haji, Muhimbili .
 
                                                            "Kutoa ni moyo si utajiri"

No comments:

Post a Comment