Friday, November 9, 2012

JE UNAFIKIRI HISTORIA KUJIRUDIA, MTOTO WA FAMILIA YA NKWABI KUTWAA TAJI LA EBSS KWA MARA NYINGINE?

Baada ya mchuano wa miezi mitatu wa kumtafuta mshindi atakayetwaa Taji la EBSS mwaka huu, hatimaye mshindi kujulikana leo, ambapo washiriki watano watachuana vikali huku kila mmoja akihakikisha ananyakua ushindi huo.

Washiriki hao watano wanochuana katika kinyang'anyiro hicho mwaka huu ni Walter Chilambo, Wababa Mtuka, Salma Abushiri, na watoto wa familia moja Nsami Nkwabi na Nshoma Ng'hangasamala.

Fainali hizo zitafanyika leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee kwa viingilio vya VVIP Tshs 70,000, VIP Tshs 30,000 na kawaida Tshs 10,000 ambapo mshindi atajinyakulia kitita cha shilingi milioni hamsini pamoja na mkataba wa kurekodi nyimbo kutoka kwa
wadhamini wakuu wa shindano hilo, kampuni ya simu za mkononi Zantel

Wasanii watakaopamba kwa burudani katika fainali hizo ni Rich Mavoko, Ommy Dimpoz, Ben Paul, Linah, Amini, Mzee Yusuf na mkewe Leyla Rashid, mshindi wa shindano hilo mwaka jana(Haji Ramadhan) Mwasiti, Ditto, Linex na Barnaba. 

No comments:

Post a Comment