Friday, November 2, 2012

HIVI NDIVYO GARI YA WOLPER ILIVYOCHOMWA MOTO

Gari hiyo inavyoonekana kwa mbele
Hii ndiyo sehemu ambayo imechomwa na ukiangalia kwa juu utaona Turubai nalo limechomwa moto na kwa maelezo ya Wolper mwenyewe anahisi mtu huyo aliyefanya tukio hilo alirusha kitambaa kilicholowanishwa mafuta na kukirusha kwenye turubai hilo kwa lengo la kuunguza gari hiyo aina ya Toyota Brevs.
Kwa nyuma gari hiyo inaonekana hivi
Kwa karibu zaidi jinsi gari hiyo ilivyochomwa.

Watu wasiojulikana wamechoma moto Gari ya Staa wa Filamu Tanzania Jackline Wolper aina ya Toyota Brevs.

Kwa mujibu wa Wolper mwenyewe tukio hilo limetokea usiku wa Oktoba 23, 2012 ambapo inahisiwa kuwa mtu huyo alitumia matambara yenye mafuta ya taa au petroli na kuyarusha ndani ya nyumba anayoishi Wolper kwa lengo la kuichoma gari hiyo.

Wolper amesema kuwa mpaka sasa hakuna mtu nayemhisi kuhusika na tukio hilo kwa kuwa katika kumbu kumbu zake hakumbuki kuwa na ugomvi na mtu yeyote ambao umepelekea tukio hilo ila anaamini kuwa mtu/watu waliohusika na tukio hilo ni wale wasiopenda maendeleo yake.
"Kiukweli siwezi kumuhisi mtu ila najua ni lazima atakua mtu asiependa maendeleo yangu ni mtu mbaya sana kwangu. Na inawezekana kabisa alipanga kuniua lakni kwa bahati nzuri siku hiyo sikua nyumbani nilikua nimesafiri." alisema Wolper.
Ameongeza kuwa amepeleka taarifa hizo katika kituo cha polisi Kawe kwa ajili ya msaada wa kiupelelezi.
Blog hii inampa pole Wolper kwa tukio hilo, vitendo kama hivi ni vitendo vya kinyama na havifai katika jamii na tunapaswa kuwa na wivu wa maendeleo na si wivu wa aina hii wa kurudishana nyuma.

Habari hii ni kwa mujibu wa Wolper mwenyewe na Blog yake ya www.jacklinewolper.blogspot.com

No comments:

Post a Comment