Thursday, November 8, 2012

RUSSELL SIMMONS ATOA DOLA ELFU KUMI KUCHANGIA FLAVIANA MATATA FOUNDATION

Mfanyabiashara mkubwa nchini Marekani Russell Simmons ametoa Dola za kimarekani 10,000(zaidi ya mil. 15 za kitanzania) kwa ajili ya kusaidia mfuko wa Flaviana Matata (Flaviana Matata Foundation).

Katika mazungumzo yao kwenye mtandao wa kijamii (Twitter) Simmons amesema anajisikia furaha kumsaidia mtu ambae ameweza kusaidia wengine nchini Tanzania.

Russel Simmons si jina geni masikioni mwa wengi kwani hapo miaka ya nyuma iliripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa mfanyabiashara huyo anatoka kimapenzi na mwanamitindo huyo lakini baadae Flaviana alikanusha habari hiyo.
Hata hivyo Uncle Russell kama wenyewe wanavyomuita ni mmoja kati ya watu waliomtengenezea njia ya kupata mkataba wa uanamitindo na kuitangaza Tanzania nchini Marekani na kwingineko.

Flaviana Matata Foundation ilizinduliwa May 21,2011 kwa ajili ya kusaidia watu wasio na uwezo, wanawake na watoto.

No comments:

Post a Comment