Thursday, November 8, 2012

SERIKALI YA JAPAN YATIA SAINI MSAADA WA SHS MIL 380 KWA AJILI YA MIRADI MIPYA YA LINDI NA MTWARA

Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaki Okada akisoma hotuba yake kwa viongozi wa mkoa wa Lindi na Taasisi ya Women in Social Entrepreneurship (WISE) ya mkoani Lindi wakati wa utilianaji saini mkataba wa makubaliano kati ya Ubalozi wa Japan na Taasisi ya WISE msaada wa ujenzi wa bweni la wasichana sekondari ya Ng'apa ya Lindi utakaogharimu shilingi Milioni  188. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Nassor Hamid Nassor.
Mkurugenzi wa taasisi Women in Social Entrepreneurship (WISE) ya mkoani Lindi, Astronaut Bagile (kushoto) akitiliana saini na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaki Okada (wa tatu kulia) msaada wa ujenzi wa bweni la wasichana sekondari ya Ng'apa ya Lindi utakaogharimu shilingi Milioni  188. Wengine wanaoshuhudia utiaji saini huo kutoka kushoto ni Meya wa Manispaa ya Lindi, Frank Maghali, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Nassor Hamid Nassor na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi,  Ashimun Mnzava.Utiaji saini huo wa makubaliano hayo ya msaada ulifanyika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi Novemba 7, 2012.

No comments:

Post a Comment