Wednesday, November 21, 2012

NISHA AKANA KUTOKA KIMAPENZI NA NEY WA MITEGO

Nisha katika pozi
Moja kati ya picha za Ney na Nisha zilizovuja

Siku chache baada ya picha za kimahaba za msanii Ney wa Mitego na Nisha kuvuja Nisha ameamua kufunguka kuhusu uhusiano uliopo kati yao.

Akizungumza katika kipindi cha Hotmix cha EATV Nisha amefunguka kuwa hakuna uhusiano wa mapenzi kati yake na Ney ila picha hizo zimetokana na movie yao mpya ambayo walikuwa wakishoot na picha hizo walizipiga wakati wa maandalizi ya movie hiyo ambayo inatarajiwa kutoka mapema mwakani.

 Aidha Nisha ameongeza kuwa picha hizo zimevuja baada ya simu waliyotumia kwa kupiga picha hizo kupotea na mtu aliyeokota simu hiyo ndiye aliyezisambaza, hata hivyo amewatupia lawama baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari kwa kukurupuka na kuandika habari kuhusu picha hizo bila hata ya kuwauliza wahusika ili wapate ukweli wa picha hizo.

No comments:

Post a Comment