Tuesday, November 13, 2012

MATOKEO YA UCHAGUZI WAJUMBE WA NEC YAVUJA

Wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM kutoka mkoani Mtwara
Mh. Wassira akiwa na baadhi ya wajumbe wa mkutano huo


MATOKEO  ya uchaguzi wa wajumbe wa NEC katika kura zilizopigwa juzi mjini Dodoma katika mkutano wa  nane wa Chama cha Mapinduzi (CCM) yamevuja.

Huku Mwenyekiti wa chama hicho kinachoiongoza Serikali, Rais Jakaya Kikwete akitangaza jana kuwa matokeo hayo yatatangazwa leo pamoja na matokeo ya nafasi za Makamu Mwenyekiti lakini tayari hadi jana mchana zaidi ya asiliamia 90 ya wajumbe walisha jua matokeo hayo na kuanza kupongezana huku yale ya wagombea wa bara yakiwekwa na idadi ya kura zao. 

Ingawa baadhi ya wajumbe wameoneshwa kushangazwa na idadi ya kura alizopata Katibu Mkuu wa Chama hicho Wilson Mukama kwa kushika nafasi ya 9 huku Steven Wasira akiwaongoza.

Wanaodaiwa kushinda nafasi 10 Zanzibar:
Mbunge wa Uzini, Mohamed Seif Khatib; Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Ali Mwinyi, Waziri wa Fedha Zanzibar, Omar Yussuf Mzee, Abdulhakim Chasama na  Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Shamsi Vuai Nahodha.

Wengine  ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Khadija Hassan Aboud, Bhaguanji Mansuria, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa na Khamis Mbeto.

Wanaodaiwa kushinda Bara

Majina ya wajumbe wa Nec walioshinda bara na kura walizopata katika mabano ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira aliyeongoza kundi hilo kwa kupata kura 2,135, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (2,093), Mwekahazina wa CCM, Mwigulu Nchemba (1,967), na Katibu wa UVCCM, Martine Shigela (1,824).

Wengine ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi (1,805), Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe (1,455), Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mathayo David Mathayo (1,414), Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome (1,207), Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama (1,174) pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana  na Michezo, Fenela Mukangara (984).

SOURCE:http://mrokim.blogspot.com

No comments:

Post a Comment