Friday, May 31, 2013

MWILI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEA UTAWASILI DAR ES SALAAM JUMAPILI BADALA JUMAMOSI

Mwili wa marehemu Albert Mangwea utawasili Jumapili badala ya Jumamosi kama ambavyo ilipangwa hapo awali.

Kwa mujibu wa kamati ya maandalizi ya msiba huo kupitia ,semaji wake Adam Juma ni kuwa, maamuzi hayo yametokana na maombi ya watanzania waishio nchini Afrika kusini kuomba kuuaga mwili wa marehemu hapo kesho.

Kufuatia mabadiliko hayo mwili wa marehemu utawasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. J.K Nyerere siku hiyo ya Jumapili majira ya saa 7.30 mchana ambapo mashabiki, ndugu, jamaa na marafiki wa Mangwea watapata nafasi ya kuuaga mwili Jumatatu kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 6 mchana katika viwanja vya Leaders Club na baadae safari ya kuelekea Morogoro kwa mazishi itaanza ambapo atazikwa siku ya Jumanne.

Hivyo ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wa Mangwea mnaombwa kujitokeza kwa wingi uwanja wa ndege ili kuupokea mwili wa marehemu na katika viwanja Leaders Club ili kuuaga mwili wa ndugu yetu, kipenzi chetu Albert Mangwea.

No comments:

Post a Comment