Monday, May 20, 2013

NGASSA AREJEA NYUMBANI YANGA ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI

Mrisho Ngassa akizungumza na waandishi wa habari.
Pichani juu ni Mrisho Ngassa akikabidhiwa jezi ya Yanga na chini akibusu Jezi hiyo.
Habari zilizotufikia hivi punde zinasema Mchezaji wa zamani wa Young African sports Club (Yanga) Mrisho Khalfan Ngassa amerejea tena Yanga na tayari amesaini mkataba wa miaka miwili muda mfupi uliopita.

Ngassa ambae alihamia Simba August 2, mwaka jana kwa mkopo akitokea Azam FC baada ya timu hiyo kutangaza kuwa iko tayari kumuuza mchezaji huyo kwa timu yoyote itakayofikia dau la dola 50,000 ambapo Yanga ilikuwa tayari kumtwaa mchezaji huyo kwa dau la Tshs mil.20 huku watani wao Simba wakiwashinda kwa dau la mil.25 na kumtwaa mchezaji huyo.




No comments:

Post a Comment