Tuesday, May 14, 2013

WAREMBO 12 WAJITOKEZA KUWANIA MISS LINDI 2013, MEI 31

Zaidi ya warembo 12 wanatarajiwa kushiriki kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka Malkia wa Mkoa wa Lindi ‘Miss Lindi 2013’ linalotarajia kufanyika Mei 31 mwaka huu katika ukumbi wa Hoteli ya Lindi Beach Resort (Lindi Oceanic Hotel).

Akizungumza na Blog hii kutoka mjini Lindi, Muandaaji wa Shindano hilo, Shaha Ramadhani kupitia kampuni ya Alliance Entertainment amesema warembo 12 wataingia Kambini Hotelini hapo chini ya Mkufunzi Zainab Mselemu ambaye alikuwa Miss Pwani 2010.

Maandalizi yote ya shindano hilo yanaendelea vyema na Milango iko wazi kwa Wadhamini kujitokeza.

Irene Veda (pichani juu) ndiye anashikilia taji hilo baada ya kulitwaa mwaka 2012. 

No comments:

Post a Comment