Friday, May 31, 2013

SERIKALI KUWAWEZESHA WAGONJWA KUTAMBUA DAWA FEKI KWA KUTUMIA SIMU ZA MKONONI


Katika juhudi za kukabiliana na ongezeko la dawa feki za binadamu serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya kimataifa ya kutengeneza dawa baridi ya Glaxo Smith Kline imezindua mpango utakaowezesha wagonjwa kutambua ubora wa dawa kupitia simu za mkononi.
Akizungumza na wadau wa sekta ya Afya Naibu waziri wa Afya Mh. Seif Rashid (pichani), amesema mpango huo unalenga kuiongezea nguvu serikali katika jitihada za kufikiwa kwa malengo ya millennia pamoja na kuleta mageuzi katika utoaji wa huduma katika sekta ya afya na kuwawezesha wananchi kuwa na uhakika wa dawa wanazozitumia.
Mkurugenzi wa Udhibiti wa Nchi zinazoendelea wa kampuni ya Kimataifa ya Glaxo Smith Kline Dkt. William Mwatu amesema utafiti uliofanywa katika nchi za Kenya na Tanzania umeonyesha kuwa wagonjwa wengi wamekuwa na hofu wa dawa wanazotumia.
Mh. Seif Amesisitiza kuwa asilimia 30 ya dawa zilizo katika maduka ya dawa baridi ni feki, kiwango ambacho kinatarajiwa kuongezeka kwa asilimi 13 kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment