Friday, May 31, 2013

BARAZA LA MITIHANI LATANGAZA MATOKEO KIDATO CHA 6


Baraza la mitihani Tanzania, leo limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha sita uliofanyika mwezi February mwaka huu..
Akitangaza matokeo hayo katika ofisi za baraza hilo Mikocheni jijini DSM, Naibu katibu mtendaji wa baraza hilo Dr. Charles Msonde amesema Jumla ya watahiniwa wa shule 40,242 kati ya watahiniwa 42,952 sawa na asilimia 93.92 wamefaulu kwa daraja la 1 hadi la nne.

Aidha Dr msonde ametaja shule 10 bora, zilizoongozwa na Marian Girls ya Pwani katika kundi la watahiniwa zaidi ya 30 ambazo ni Mzumbe Secondary school, Feza Boys, Ilboru, Kisimiri, St. Mary's Mazinde juu, Tabora Girls, Igowole, Kibaha Secondary school na Kifungilo Girls.

Pia ametaja watahiniwa waliofanya vizuri katika masomo mbalimbali, Kwa upande wa Sayansi aliyeongoza ni Erasmi Inyanse aliyekuwa akisoma PCM kutoka Ilboru shule ya Arusha, kwa masomo ya biashara wa kwanza ni Erick Robert Mulogo kutoka Tusiime ya DSM kombi ya ECA, na kwa masomo ya lugha na sayansi ya Jamii ni Asia Idd Mti kutoka Barbro-Johansson ya DSM alikuwa akisoma HGE.

No comments:

Post a Comment