Monday, May 27, 2013

MICHEZO YA UMISETA YAZINDULIWA LEO HII MKOANI LINDI

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa Afisa elimu, Taaluma Mkoa wa Lindi Bwana Sarufu Kakama (pichani juu)
Sehemu ya wanamichezo 640 kutoka katika Halmashauri 6 za Wilaya zinazounda Mkoa wa Lindi.

Ufunguzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo na Sanaa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) mkoani Lindi umefanyika rasmi leo katika Viwanja vya shule ya sekondari Lindi.

Uzinduzi huo wa michezo ya Umiseta iliyojumuisha wanamichezo 640 kutoka katika Halmashauri 6 za Wilaya zinazounda Mkoa wa Lindi ambapo mashindano hayo ya michezo hiyo yanafanyika kwa siku nne mfululizo huku yakitoa fursa ya kuchagua wanamichezo watakaoshiri katika michezo hiyo Kanda ya Kusini.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Ambae pia ni afisa elimu Taaluma Mkoa wa Lindi,Sarufu Kakama amesisitiza wanamichezo wote kucheza na kushindana bila kuumizana na kucheza kwa upendo na kuzingatia nidhamu kama ambavyo wawapo mashuleni mwao ili kujenga mshikamano baina ya wao kwa wao ikiwemo na walimu wao.

Aidha Kakama alieleza mkoa wa Lindi ulivyojipanga katika michuano hiyo iliyoanza leo ngazi ya mkoa kuelekea kanda itakayofanyika Hivi karibuni mkoani humo
Nae Kaimu Afisa Utamaduni Manispaa ya Lindi,Mwl Alice Choaji licha ya kuelezea michezo kama masomo mengineyo na kwa kuzingatia somo hilo kwasababu michezo ni ajira, michezo hutatua migogoro katika jamii mbalimbali, michezo hudumisha utamaduni wa nchi na makabila mbalimbali ikiwemo kuibua vipaji vya watoto alieleza.

Katika  mashindano hayo kuna jumla ya michezo saba ikiwemo soka wavulana na wasichana, netiboli kwa wasichana, riadha wavulana na wasichana kuanzia mita 100 hadi 5000, basketiboli wavulana na wasichana, wavu wavulana na wasichan na tufe ambapo michezo hiyo itakuwa kifanyika kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi 11:30 jioni kwenye viwanja hivyo vya Lindi Sekondari na Mtanda kwa Mpira wa Miguu

SOURCE:Abdul Aziz video-Lindi

No comments:

Post a Comment