Tuesday, May 14, 2013

WANAFUNZI SHULE YA SEKONDARI MANZESE WAANGUKA NA KUPOTEZA FAHAMU

Mmoja kati ya wanafunzi walioanguka shuleni hapo 
Baadhi ya wanafunzi hao wakiwa katika hali mbaya.
Zaidi ya wanafunzi 40 wa shule ya sekondari Manzese jijini Dar Es Salaam, wameanguka na kupoteza fahamu wakiwa  shuleni  huku wengine wakitoka madarasani na kukimbia ovyo.

Tukio hilo limetokea leo majira ya saa nne asubuhi ambapo alianza mwanafunzi mmoja kupiga kelele na kuanguka wakati wakiendelea na masomo na baadae kutolewa nje ya darasa lakini jambo la kushangaza ghafla wanafunzi wengine zaidi ya 40 nao walianza kupiga kelele na kupigana kama watu waliorukwa na akili na kuanguka.

Hata hivyo wakati hayo yakiendelea uongozi wa shule hiyo uligoma kuzungumzia tukio hilo pale waandishi wa habari walipohitaji ufafanuzi wa tukio hilo.

No comments:

Post a Comment