Wednesday, May 15, 2013

D'BANJI APATA SHAVU LA KUWA BALOZI WA BENKI YA VIWANDA NIGERIA

Pichani ni mwanamuziki D'banji akiwa amesimama na Mkurugenzi mwendeshaji na Afisa mtendaji mkuu wa benki ya viwanda Nigeria bi. Evelyn Oputu.

Mwanamuziki nyota wa nchini Nigeria D'banj ameteuliwa kuwa balozi mpya wa benki ya viwanda huko Lagos, Nchini Nigeria.

Hii ni nafasi nyingine ya msanii huyo aliyepata umaarufu kwa ngoma zake kali kama vile Fall in Love, Oliver Twist na nyinginezo kula nafasi hiyo ambayo inamuweka katika nafasi nzuri zaidi kimataifa, ambapo baada ya kupata nafasi hiyo aliwajuza mashabiki wake kupitia account yake ya Twitter kuwa ametajwa kushika nafasi hiyo ya ubalozi wa benki hiyo.
 
Kila la kheri d'banji katika nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment