Thursday, May 23, 2013

HALI MKOANI MTWARA YAENDELEA KUWA TETE, RAIS ATOA TAMKO, BUNGE LAAHIRISHWA TENA WATU 91 WATIWA MBARONI

Wakati hali ikizidi kuwa tete Mkaoni Mtwara kufutia vurugu ziliyoanza jana Mkoani hum,o Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ametoa amri  kwa Jeshi la olisi kuhakikisha wahusika wote wa vuugu hizo kusakwa na kutiwa nguvuni mara moja.
 Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa barabara kuu ya Iringa-Dodoma katika eneo la Kizota mkoani Dodoma  Rais Kikwete  alisema wote waliohusika na vurugu hizo watasakwa na kuchukuliwa hatua kali.
Rais Kikwete alisema rasilimali inayopatikana mahali popote pale nchini inatakiwa kutumiwa na Watanzania wote.
Wakati huo huo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Anna Makinda ameliahirisha tena bunge leo asubuhi baada ya jana jioni kuitaka Serikali ije na ripoti ya tukio hilo ambapo leo ameitaka kamati ya uongozi ya Bunge iendelee kukutana ili kutoa maamuzi na tamko kuhusu vurugu hizo zinazoendelea Mkoani humo na kusababisha kifo cha mtu mmoja na uharibifu wa mali ikiwemo kuchomwa moto kwa nyumba za viongozi wa serikali,chama cha mapinduzi na nyumba ya mwandishi wa habari wa TBC Kassim Mikongoro.
Hata hivyo mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini umesimamishwa kwa muda mpaka ufumbuzi wa tatizo la vurugu hizo utakapopatiwa ufumbuzi ambapo Kesho Bunge litajadili bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya Afrika Mashariki.
Aidha Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara ACP Linus Sinzumwa amesema Jeshi la polisi mkoani humo linawashikilia watu 91 kwa tuhuma za kuhusika na vurugu hizo na hatua itakayofuata ni kufanya nao mahojiano ili kubaini chanzo cha vurugu hizo na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi limejipanga ili kudhibiti vurugu hizo na kurejesha hali ya amani.

No comments:

Post a Comment