Monday, May 20, 2013

MHESHIMIWA SUGU ACHAFUA HALI YA HEWA MJENGOZI

Spika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda amesitisha kikao cha bunge na kuiruhusu kamati ya kanuni za bunge kuijadili hotuba ya bajeti ya kambi ya upinzani kuhusu wizara ya habari, utamaduni na michezo.

Hayo yametokea baada ya Mheshimiwa Joseph Mbilinyi (Pichani) kuanza kuwasilisha hotuba hiyo     ambayo imedaiwa kuwa na maneno ya uchochezi.

Bunge limeahirishwa mpaka saa 11 jioni ambapo kamati ya kanuni ya Bunge itakapoipitia hotuba ya bajeti ya kambi ya upinzani  na kujiridhisha kwamba haina maneno ya uchochezi.

Hii si mara ya kwanza  katika Bunge hili la mkutano wa 11 kusitisha hotuba za upinzani na kuitaka kamati ya kanuni ipitie upya.

No comments:

Post a Comment