Monday, May 20, 2013

MBUNGE WA IRINGA MJINI MCH. PETER MSIGWA AMEACHIWA KWA DHAMANA

Pichani juu ni Mchungaji Peter Msigwa akiikishwa mahakamani
Watuhumiwa wengine 60 wakishuka kwenye karandinga la Polisi kuelekea Mahakamani huku Polisi wakiimarisha ulinzi katika eneo hilo.

WATUHUMIWA 60 wa vurugu kati ya wamachinga na polisi mjini Iringa akiwemo Mbunge  wa  Jimbo  hilo, Mchungaji Peter Msigwa wameachiwa kwa dhamana baada ya walisomewa mashitaka matatu  huku mbunge  akisomewa shitaka la  kushawishi  watuhumiwa hao kufanya  vurugu.
  
Watuhumiwa  wote  wamekana mashitaka  dhidi yao na baadae utaratibu  wa dhamana  ukafanyika mbele  ya mahakama ya  hakimu mkazi  wa wilaya ya  Iringa, Mheshimiwa  Godfrey Isaya.
 
Mashitaka waliyosomewa watuhumiwa ni pamoja na shitaka la kwanza la mbunge ambalo ni kushawishi kufanya vurugu, huku  wengine  wote  makosa yao yakiwa ni kufanya mkutano bila kibali, kuharibu mali kinyume na sheria ni  kufanya  vurugu.

No comments:

Post a Comment