Monday, May 20, 2013

INDIA NA CHINA ZAAFIKIANA KUHUSU MPAKA

Waziri mkuu wa China (PICHANI KULIA) yupoNchini  India kwa ziara yake ya kwanza ya nje inayoonekana kugubikwa na mzozo wa muda mrefu wa mpaka kati ya nchi hizo mbili za bara la Asia.
Ziara ya waziri mkuu huyo wa China inajiri wiki kadhaa baada ya kuwepo malalamiko kutyoka kwa umma kufuatia India kukishutumu kikosi cha China kuingia ktika maeneo yake.

Zaidi ya miaka hamsini iliyopita tangu nchi hizo zilipopigana vita vya muda mfupi, bado nchi hizo hazijakubaliana kuhusu mipaka yao, na India inatuhumu China kwa kudhibiti sehemu kubwa ya ardhi yake.Mkwamo huo hatimaye ulitatuliwa kwa amani , lakini umezua mtazamo mwingine wa hatari inayotokana na mzozo kati ya nchi hizo mbili zenye idadi kubwa ya watu.
Waziri mkuu wa India alimpokea mwenzake wa China kwa tabasamu na waziri mkuu wa China akisisitiza kwamba lengo kuu la ziara yake ni kujenga imani kati ya nchi hizo mbili.
Aidha Li Keqiang amesema kuwa India na China lazima ziimarishe juhudi zake kutuliza mzozo wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili huku akiahidi kuunga mkono juhudi za amani na utulivu
SOURCE:BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment