Tuesday, May 21, 2013

SPIKA WA BUNGE AAMURU KUFUTWA KWA HOTUBA YA KAMBI YA UPINZANI ILIYOSABABISHA BUNGE LISITISHWE JANA ASUBUHI


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Anne Makinda, ameamuru kambi ya upinzani kuyaondoa maneno yote yaliyomo kuanzia ukurasa wa kwanza mpaka wa 14 katika hotuba rasmi ya Kambi ya upinzani iliyosmwa na mbunge wa Mbeya Mjini, Mh. Joseph Mbilinyi "Sugu" ambaye ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Mh. Makinda ametoa amri hiyo kufuatia kamati ya kanui ya Bunge kujadili hotuba hiyo na kubaini kuwa kauli za uchochezi na kusema kuwa Bunge siyo sehemu ya kugombanisha wananchi, hivyo maneno yote ya uchochezi hayaruhusiwi.
 
Katika hotuba hiyo, Mh. Mbilinyi aliishutumu serikali kuhusika na kuteka nyara waandishi wa habari, kauli iliyopelekea Spika Makinda kuahirisha Bunge.


No comments:

Post a Comment