Monday, May 27, 2013

FEZA KESSY NA NANDO WAWAKILISHI WA TANZANIA KATIKA SHINDANO LA BIG BROTHER 2013

Mwakilishi kutoka Tanzania Nando akihojiwa na Mtangazaji wa kipindi hicho Ik wakati wa uzinduzi wa show hiyo, Kushoto patna wa Nando Mshiriki kutoka Namibia Cleo.
Mwakilishi mwingine kutoka Tanzania Feza Kessy, akitambulishwa kwa patner wake kutoka Ghana Elikem wakati wa uzinduzi wa shinado hilo.
Feza Kessy akiwasalimia mashabiki waliojitokeza katika uzinduzi wa shindano hilo.

Kile kitendawili cha nani ataiwakilisha Tanzania katika shindano la Big Brother The chase 2013, kimeteguliwa jana katika uzinduzi wa shindano hilo uliofanyika jana jijini Johannesburg Afrika ya Kusini huku Tanzania ikiwakilishwa na Feza Kessy na Nando.

Wengi wameonyesha kustaajabu baada ya kuwaona washiriki hao kinyume cha matarajio ya wengi ambapo magazeti mbalimbali yaliripoti kuwa mastaa Wema Sepetu, Baby Madaha au Jackline Pentzel ndiyo wangeiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo mwaka huu ingawa wahusika wenyewe walipoulizwa walikanusha madai hayo.

Kila la kheri Feza na Nando tunaamini ushindi utarudi Tanzania.  

No comments:

Post a Comment