Tuesday, October 25, 2011

YVONNE CHAKACHAKA NA YOUSSOU N'DOUR KUTOA WIMBO UNAOELIMISHA KUHUSU MADAWA FEKI

Yvonne Chakachaka(Princess of Africa)

Youssou N'dour


Wanamuziki Nguli barani Afrika, Yvonne Chakachaka na Youssou N'dour wanatarajia kuzindua wimbo wao mpya walioupa jina la "PROUD TO BE" ukiwa na lengo la kuielimisha jamii ya Afrika kuhusiana na Madhara ya matumizi ya madawa Feki.

Uzinduzi wa wimbo huo utafanyika October 27, 2011 katika Hotel ya Hilton jijini Nairobi, Kenya. Yvonne Chakachaka anayefahamika pia kama Princess of Africa atafanya Onyesho saa 11:00 asubuhi ambapo pia atashiriki katika mkutano na waandishi wa habari.

Kutoka kwa Afrokija: Madawa haya Feki yanaweka maisha yetu hatarini, hivyo tunatakiwa kuwa makini na dawa hizi ili kujiepusha na madhara yanayoweza kutokea maana si wote ambao hupoteza maisha, tumeshuhudia ndugu zetu wengi tu wakipata ulemavu wa kudumu na hata maradhi ya muda mrefu kutokana na matumizi ya dawa hizo Feki, Hivyo tunapaswa kuwa makini!!

Kwa habari zaidi, tembelea:www.safemedicines.org

No comments:

Post a Comment