Monday, October 17, 2011

JE UNAWEZA KUMPATA MTU MWENYE MAPENZI YA AINA HII KATIKA DUNIA YA LEO?

Wapenzi na wachumba katika dunia hii ni wengi sana, lakini wakweli ni wangapi kati yao? Ni watu wangapi ambao husema kweli katika mapenzi yao? Ni wangapi ambao humaanisha wanachokisema? Ni wangapi ambao wanaweza kuendelea kubaki na wapenzi wao pindi wapenzi hao wanapopata matatizo kama vile ulemavu au ugonjwa usiotibika?

Hii ni stori pekee ya mapenzi ya kweli niliyowahi kuisikia...........

Huyu mama ni mtu mwenye bahati sana ( Anaitwa Rosemarie "Rose" Siggins)

Huu ni mfano mzuri wa Familia ya kuigwa

Kwa kweli kwa namna hii huyu mama anaweza kuishinda hali yake ya kuwa mlemavu na kujihisi yuko sawa na wengine

Ni mama wa watoto wawili kama unavyoona na anafurahia maisha na familia yake

Mama na wanae
Akimnyonyesha mwanae mwenyewe 

Matembezini na familia
Wakiwa shopping na maisha yanaendelea anaenjoy zaidi ya wewe ambae umetimia

Pamoja na yote mwisho wa siku jukumu la kumlea mtoto wake linamsubiri na anaweza kulimudu kama kawaida, kama umegundua ana kama kabaiskeli hivi kakutembelea

Kiukweli huu ni mfano mzuri sana wa kuigwa kwa huyu baba na kama wapenzi wote tungekuwa hivi basi maisha yangekuwa na furaha na yasiyo na stress wakati wote, lakini upande wa pili huku ni full stress aiseh mpaka wengine wanadiriki kusema wao mapenzi basi lakini mwisho wa siku wanagundua kuwa haiwezekani na yataka moyo kumudu uamuzi huo na hatimae wanarudi tena kundini... Ila kikubwa ambacho nimejifunza katika ulimwengu huu wa mapenzi ni uvumilivu na kuaminiana tu basi hiyo ndiyo dawa ya kutibu ugonjwa huu wa stress katika suala zima la mapenzi.

UJUMBE HUU UENDE KWA WOTE WALIO KWENYE NDOA NA WALE AMBAO WAKO KWENYE UHUSIANO WA KAWAIDA TU, MAANA KUNA KITU CHA KUJIFUNZA HAPO KWETU SISI SOTE!!!!

Thanks my Boy Andrew Zomari kwa habari hii.

No comments:

Post a Comment