Monday, October 24, 2011

WEMA NA DIAMOND NINA MACHACHE KWA AJILI YENU

Sarakasi za 'Love-Cartoon' kali star wa Bongo Flava,Naseeb Abdul aka Diamond baada ya kutangaza kummwaga Wema Sepetu (Miss TZ 2006-2007) kwa sasa zimefunguliwa upya kuwa busara za mama mzazi wa Diamond,Sanura Khassim ziliokoa jahazi kwa kumlazimisha mwanaye arudiane na Wema ili mambo yasiharibike....
Imefunguliwa kuwa baada ya Wema kupiga simu na 'kulia lia' kwa mkwe kuwa atakunywa sumu,Mama Mkwe aliwaita Wema na Diamond na wajomba zake nyumbani kwake,ili wazungumze na baada ya mvutano wa muda mrefu,wajomba na Mama walikomaa Diamond alinywea akasalimu amri mbele ya wakubwa na kurudiana na lovi-davi wake aliye-make sana headlines kwa kutoka na Ma-Star wa bongo kuanzia....Steven Kanumba, Charles Baba,Hartmann Mbilinyi na Jumbe Yusuf.

SOURCE: chini ya carpet

Kutoka kwa Afrokija: Mi nadhani hivi vitu ambavyo vinaendelea kwa sasa ni vya kudhalilishana, kama mmeamua kupendana basi mtulie na muonyeshe hayo mapenzi yenu kuliko kuanika mambo yenu kila siku, coz kuna Couples nyingi tu hapa bongo lakini hatuoni wakidhalilishana kama mnavyofanya nyie, Binafsi naamini kuwa endapo unampenda mwenzi wako utamlinda na hutopenda apate aibu na kudhalilishwa kila kukicha hata kama amekukwaza.. Nampenda sana Wema pamoja na yote yanayomtokea ila Diamond unapaswa kutunza heshima ya mwenzako usichukulie udhaifu wake wa kukupenda kwa kumtia aibu kwenye vyombo vya habari kila kukicha.

No comments:

Post a Comment