Friday, October 21, 2011

MKUBWA NA WANAWE NDANI YA AFROBEAT JUMAMOSI HII

Kijah na mkubwa Fella katika Interview

Baadhi ya wanawe Fella kulia ni Aslay ambae anakimbiza kwa sasa na wimbo wake naenda kusema huyo mwngine ndo yuko mbioni kutoka lakini yeye ni upande wa Taarabu

Hapa wanawe wakiwa Stejini, kitu ambacho kilinishangaza ni kuona Aslay akiimba Taarab yaani huko ndo anakaza zaidi ya huku ambako tumemzoea.. Jamani huyu mtoto ana kipaji cha hali ya juu namtabiria mazuri na atafika mbali sana coz siyo tu ana kipaji ana nidhamu na heshima ya hali ya juu sana tofauti na watoto wengine

Hii picha haikuwa nzuri kwa sababu ya mandhari yenyewe, ni Leah Moudy na Band yake mpya ya Q-Band ambayo anaimiliki yeye na mchumba wake Siz -Q, nao pia utawaona kwenye Afrobeat Jumamosi hii.
Ili kuona mengi kuhusiana na hayo niliyokudokezea hapo juu usikose kuangalia Afrobeat hapo kesho Jumamosi saa moja jioni..

No comments:

Post a Comment