Thursday, June 30, 2011

MSONDO NGOMA MUSIC BAND KUWEKA KAMBI NDANI YA KIJIJI CHA MAKUMBUSHO

(PICHANI juu na chini ni Baadhi ya wanamuziki wa Msondo ngoma wakionyesha vitu vyao jukwaani)

Bendi kongwe ya muziki wa Dansi nchini, (MSONDO NGOMA) Baba ya muziki,IJUMAA hii inatarajia kufanya onyesho maalum lijulikanalo kwa jina la MTANZANIA JIVUNIE katika kijiji cha Makumbusho JIJINI DAR ES SALAAM.

Meneja wa Bendi hiyo SAID KIBIRITI amesema onyesho hilo maalum limeandaliwa na bendi yake kwa kushirikiana na uongozi wa kijiji cha MAKUMBUSHO, na Baada ya hapo bendi hiyo itakuwa ikipiga Show katika kijiji hicho kila siku ya IJUMAA

MAALIM GURUMO(Kiongozi wa Bendi)

Bendi ya Msondo ngoma kwa sasa inatamba na kibao kipya kijulikanacho kama SULUHU kilichotungwa na SHABAN DEDE, Hivyo idadi ya nyimbo mpya za msondo kufikia TANO ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya ALBUM yao mpya

SAID MABERA(Mpiga gitaa la Solo wa MSONDO)

KIBIRITI amewaomba wapenzi wa Bendi hiyo kujitokeza kwa wingi ili kuipa SUPPORT Bendi yao hiyo


ROMARIO kazini

No comments:

Post a Comment