Saturday, June 18, 2011

HALI YA BAMBO BADO NI TETE

Muigizaji na mchekeshaji mkongwe bongo ambae kwa sasa ni muajiriwa wa EATV kupitia ZE COMEDY SHOW, Dickson Makwaiyo a.k.a Bambo, ambae wiki iliyopita aliripotiwa kupata ajali ya pikipiki na kusababisha kuvunjika kwa mfupa sehemu ya goti hali yake bado si nzuri.
Pichani juu ni pikipiki na gari iliyosababisha ajali ya Bambo

Hali ya Bambo ilikuwa inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji lakini katika hali isiyo ya kawaida habari zilizotufikia leo zinasema kuwa Bambo alianza kutokwa damu masikioni na baadae kufanyiwa uchunguzi zaidi na majibu zaidi yatapatikana kesho


Mtanga na Kicheko kutoka ZE COMEDY ya EATV wakimjulia hali Bambo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini DSM.

No comments:

Post a Comment