Tuesday, June 28, 2011

VIMWANA MANYWELE 2011 WATAMBIANA

Wakati shindano la kumsaka Manywele kimwana wa Twanga pepeta likielekea katika hatua ya Fainali, Vimwana  kumi  walioingia katika hatua hiyo wameibuka na kutambiana kuwa kila mmoja ndiye mwenye uwezo na vigezo vya kuibuka na ushindi
Nae Matron wa Vimwana hao ambae pia ni kimwana mstaafu wa mwaka 2007 ambae alishika nafasi ya pili HUSNA IDD a.k.a SAJENT amesema hana mashaka na vimwana hao kwa kuwa kila mmoja amefanya maandali ya kutosha na yeyote kati yao anaweza kunyakua ushindi
Kwa upande wake Mratibu wa shindano hilo MAIMARTHA JESSE amesema kila kitu kimekamilika ikiwa ni pamoja na zawadi ya duka la vipodozi lenye thamani ya Shs Mil. 5, kinachosubiriwa ni siku ya mpambano ili zijulikane mbivu na mbichi. Fainali hiyo ya manywele kimwana wa Twanga pepeta itafanyika Tar 08.07.2011 katika ukumbi wa Ubungo Plaza kwa UDHAMINI mkubwa kabisa wa AFROBEAT ya EATV na  AFROSUNDAY ya EAST AFRICA RADIO

No comments:

Post a Comment