Tuesday, June 28, 2011

WAKONGWE WA MUZIKI TANZANIA KUTOA ALBUM YA NYIMBO ZA ZAMANI

(Abdul Salvador a.k.a Father Kidevu)
Wanamuziki wakongwe Tanzania wamejipanga na kuamua Kutoa Album ya nyimbo za zamani, akizungumza na kipindi cha AFROBEAT cha EATV mmoja kati ya wanamuziki hao aliyetamba enzi hizo kwa umahiri wake wa kupiga Kinanda kwa kutumia kidevu ABDUL SALVADOR a.k.a FATHER KIDEVU amesema nyimbo watakazorekodi ni zile zilizotamba miaka ya 1961 mpaka 1991, wameamua kufanya hivyo katika kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania. Ameawataja baadhi ya wakongwe waliomo katika mpango ni pamoja na Kanku Kelly, Mzee Gururmo,, John Kitime, King Kikii, Ndalla Kasheba na wengineo.
Father kidevu na Kanku Kelly wa KILIMANJARO CONNECTION
Wazee wakiwa mazoezini
Babu njanje mazoezi yakiendelea
Mzee Gurumo wa MSONDO NGOMA
King Kikii na Ndalla Kasheba
Baadhi ya Wakongwe wa Muziki TZ katika picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment