Thursday, June 23, 2011

M-NET YAZINDUA AFRICA MAGIC SWAHILI


M-NET AFRICA wameanzisha kituo kipya cha kurushia matangazo ambacho kimezinduliwa jana kinachofahamika kwa jina la AFRICA MAGIC SWAHILI.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa M-NET Biora Alabi, kituo hicho kitakachoanza rasmi Julai mosi kitakuwa kikirusha matangazo yake kwa Lugha ya kiswahili ili kuikuza Lugha hiyo, lakini pia itaonyesha Filamu na muziki wa Kiswahili tu.

Wawakilishi wa M-NET katika kukamilisha uzinduzi huo

Waalikwa waliohudhuria hafla hiyo ambayo imefanyika katika hotel ya MOVENPICK


Upande wa Tasnia ya Filamu nao hawakubaki nyuma walikuwepo kuwakilisha, hapo juu ni JB moja kati ya waigizaji ambao wananifurahisha sana

Aunt Ezekiel nae kama kawaida yake hapendi kuhadithiwa lazima ajionee mwenyewe.

Kanumba The Great mmoja kati ya waigizaji bongo nae alikuwepo, hapo akifafanua jambo


The Greatest nae akiwakilisha akiwa na Cloud

Mama lao katika movie Suzan Lewis nae akiwaongoza wanae

Mtu maarufu kwa kuiga sauti za watu Steve Nyerere nae akitema cheche zake

KWA WALE WAPENDA MOVIE ZA KIBONGO KAMA MIMI KAZI NI KWENU JAMANI KUIFUATILIA TU AFRICA MAGIC SWAHILI

No comments:

Post a Comment