Monday, June 27, 2011

AKUDO IMPACT KUTAMBULISHA NYIMBO ZAO MPYA

Bendi ya muziki wa Dansi, Akudo Impact a.k.a Vijana wa masauti wanatarajia kutambulisha nyimbo zao mpya zipatazo tano hivi karibuni
Akizungumza na kipindi cha AFROBEAT kupitia EATV kinachokwenda hewani kila JUMAMOSI saa 1 Kamili JIONI, Rais wa Bendi hiyo CHRISTIAN BELLA amesema AKUDO bado iko imara tofauti na uvumi uliopo kuwa inaweza kuvunjika.
Bella ameongeza kuwa mashabiki wasisikilize maneno hayo ambayo hata yeye (BELLA) hajui yametokea wapi na wakae tayari kupokea nyimbo zao mpya zikiwemo umejificha wapi na umefulia ambazo zinatamba katika vituo mbalimbali vya Redio hapa nchini.....    ILI KUZISIKIA NYIMBO HIZO, FUATILIA AFROSUNDAY YA EAST AFRICA RADIO KILA JUMAPILI SAA 12 KAMILI JIONI



No comments:

Post a Comment