Wednesday, June 29, 2011

JAMANI TUTOE SUPPORT KWA NGOMA ZETU ZA ASILI


(Hapo juu na chini ni kikundi cha Jivunie kikitoa burudani )
Kuna tabia za baadhi ya watu kuona kuwa ngoma za asili ni kitu cha ajabu sana na wale wanaopenda kuhudhuria maonyesho ya ngoma hizo ni washamba au watu waliopitwa na wakati.
Mi nafikiri wenye haya mawazo ndo washamba na wamepitwa na wakati kwa kuthamini vitu vya kigeni, jamani utandawazi usitufanye tudharau vya kwetu tutakuwa watumwa.. Jamani badala ya kumalizia Weekend zetu kwenye CLUBS mbalimbali kila siku basi si vibaya siku moja moja tukipita kwenye hizo ngoma..
Kuna vikundi vingi tu vya ngoma ambavyo vinatoa burudani katika sehemu mbalimbali kama vile kijiji cha MAKUMBUSHO na ukipita utakuta wazungu kibaaoo na wabongo wa kuhesabu, tubadilike jamani na tuwape Support ndugu zetu hawa........     PICHA KWA HISANI YA michuzi.blogspot.com

No comments:

Post a Comment