Thursday, September 22, 2011

FAMILIA YA DR. REMMY ONGALA YAANDAA TAMASHA LA KUMUENZI BABA YAO

Mtoto wa Marehemu Dr Remmy Ongala, Aziza Ongala (kushoto)

Marehemu Dr. Remmy Ongala
Familia ya marehemu Dr. Remmy Ongala imeandaa sherehe Tamasha la kumbukumbu ya baba yao litakalofanyika Tar 10 Desemba katika viwanja vya Leaders jijini Dar Es Salaam
.
Akizungumza jijini London mtoto wa Dr. Remmy Aziza Ongala amesema wameamua kuandaa Tamasha hilo kwa ajili ya kumuenzi na kumkumbuka baba yao kwa kusherehekea Muziki wake kwa kuwa ingawa yeye(baba yao) ameondoka lakini kazi yake ya muziki bado upo na haina mwisho.

Aziza amesema kuwa kwa upande wake ni kazi ngumu sana kuandeaa Tamasha hilo kwa kuwa hajawahi kufanya kitu kama hicho na hii ni mara yake ya kwanza lakini kwa msaada wa mume wake na familia nzima ya Dr. Remmy anaamini jambo hilo litafanikiwa kwa kuwa Tamasha hilo linahusisha Familia nzima.

Hata hivyo baada ya Tamasha hilo wana mpango wa kuanzisha Dr. Remmy Ongala Foundation na ambapo wanatarajia kuianzisha mwaka ujao 2012 na wataanza kwa kutafuta na kusaidia watoto wenye vipaji na baadae wanawake kwa kuwa wanaamini kuwa ukimsaidia mwanamke umesaidia Taifa.

Source:Michuzi Blog!!

No comments:

Post a Comment